SALA YA KUOMBEA SINODI YA MAASKOFU:
Tunasimama mbele yako ewe Roho Mtakatifu
Tunapokusanyika pamoja kwa jina lako
Wewe pekee unayetuongoza
Weka masakani yako ndani ya nyoyo zetu;
Utufundishe njia ya kupita na jinsi ya kuenenda
Sisi ni dhaifu na wenye dhambi
Usiruhusu tuendelee kuchochea machafuko.
Usiruhusu ujinga utuongoze kwenye njia mbaya
Wala utepetevu usiathiri matendo yetu
Utuwezeshe ndani yako tuwe na umoja
Ili tuweze kusafiri pamoja hadi uzima wa milele,
Wala tusipotee mbali kutoka njia ya kweli na iliyo sahihi,
Tunaomba yote hayo kwako wewe ufanyae kazi kila mahali na kila wakati,
Katika ushirika wa Baba na Mwana, milele na milele.
Amina.